Jinsi ya Kuongeza Kinga ya Mwili Kupambana na Corona Mpya


 Wakati wimbi jipya la maambukizi ya virusi vya Corona yakizidi kuwa tishio duniani kote, utafiti wa Kisayansi umeendelea kuonesha kwamba watu wenye kinga imara ya miili yao, wanayo nafasi kubwa ya kupona hata baada ya kuambukizwa virusi hivyo vinavyosababisha homa kali ya mapafu.

 


Katika mahojiano na Tabibu Riziki Nkya, Mkurugenzi wa Kliniki ya JKBRS iliyopo Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam, aliyebobea katika matibabu ya tiba asili na lishe, ameeleza mambo mbalimbali yanayoweza kuongeza kinga ya mwili ya mtu bila kujali umri wake.

 

“Kabla ya kuanza kueleza mbinu hizo, ni vyema nikaeleza kuhusu dawa ambazo zinazalishwa na JKBRS kwa kutumia mimea na matunda ambazo zinaweza kuongeza kinga ya mwili kwa kasi kubwa zaidi.

 

“Tunayo dawa iitwayo Immuno Booster ambayo ni virutubisho asilia vyenye uwezo wa kuongeza madini ya Calcium na Vitamini C. Pia virutubisho hivi husaidia kukinga na kuulinda mwili dhidi ya saratani, maambukizi ya virusi ikiwemo Flu, SARS, Covid 19 na kujikinga na uvimbe na miwasho mbalimbali mwilini.

 

“Kama hiyo haitoshi, Immuno Booster inasaidia kuongeza kinga kwa watu wenye aleji mbalimbali za mafua, ngozi na kubanwa na kifua na hata watu wenye matatizo ya kifafa huwasaidia sana,” anaeleza Tabibu Riziki.

 

Kuhusu mambo yanayoweza kuongeza kinga ya mwili ukiachanana Immuno Booster, Tabibu Riziki anaeleza kuwa ulaji wa mboga za majani na matunda, unatajwa kuwa chanzo cha uzalishaji mzuri wa seli nyeupe za damu ambazo ndizo zinazofanya kazi ya kuulinda mwili dhidi ya maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

 

Anaeleza kuwa unaweza pia kutumia madini ya Zinc, Vitamin C au dawa ya ZINCOV ambayo huongeza madini haya kwa kasi kubwa mwilini ambayo pia inapatikana kwenye ofisi zao.

 

“Ofisi zetu zipo Ubungo Plaza, ‘ground floor’ kwa jijini Dar es Salaam lakini dawa zetu zinapatikana nchi nzima kupitia kwa mawakala wetu. Unaweza kuwasiliana nami kwa namba za simu 0744111115 au 0753185 592,” anahitimisha Tabibu Riziki.

1 Comments

Previous Post Next Post