Wasafi tv yapunguziwa mda wa adhabu na TCRA

 Wasafi tv yapunguziwa mda wa adhabu na TCRA

Wasafi tv yapunguziwa mda wa adhabu na TCRA

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) leo Feburuari 4, 2021, imesema imetafakari uamuzi wake wa kuifungia kwa muda wa miezi sita Wasafi TV  baada ya kituo hiko kuwasilisha maombi na vielelezo zaidi ikiomba mamlaka kupitia upya uamuzi uliotolewa.

 

Taarifa ya TCRA imeeleza, Wasafi TV iliwasilisha ushahidi kuonyesha endapo ushahidi huo ungewasilishwa wakati wa usikilizwaji, mamlaka isingeweza kutoa adhabu hiyo. Pia, walikiri kurusha matangazo mubashara kinyume na masharti ya leseni.

 

Wasafi TV itatumikia adhabu hadi mwisho wa mwezi huu Februari 28, 2021, na imetakiwa kuzingatia masharti ya leseni. Ikishindwa au kukaidi uamuzi, TCRA imesema hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post