Serikali Yasitisha Bei Mpya ya Vifurushi vya Intaneti


SERIKALI YASITISHA BEI MPYA ZA MATUMIZI YA VIFURUSHI VYA INTANETI zilizoanza kutumika leo Aprili 2, 2021 na mitandao yote ya simu na kuzua sintofahamu miongoni mwa watumiaji kutokana na bei yake kuwa kubwa tofauti na matarajio ya wananchi ambao waliahidiwa bei ingepungua.

 

“Tumesitisha matumizi ya gharama mpya za vifurushi hadi hapo itakapotangazwa baadaye. Lakini, hili litahusu vifurushi vya data pekee na vile vya sms na kupiga vitaendelea kama kawaida.” – Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma wa TCRA, Semu Mwakyanjala.

Post a Comment

Previous Post Next Post